Wednesday, February 17, 2016

Anonymous

Huyu Ndio Atakayezihukumu YANGA vs SIMBA SC

Refa (2) 
Mwamuzi Jonesia Rukyaa (28)  kuwa ndiye atakayezihukumu Yanga na Simba
Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
SIMBA na Yanga, Jumamosi hii zinashuka uwanjani kuwania pointi tatu katika mchezo wa Ligi Kuu Bara utakaopigwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo, jana Jumanne Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lilimtangaza Jonesia Rukyaa kuwa ndiye atakayezihukumu timu hizo mbili katika mechi hiyo inayotarajiwa kuwa na ushindani mkubwa.

Rukyaa mwenye umri wa miaka 28, atashuka uwanjani akiwa na kumbukumbu ya kuzichezesha timu hizo kongwe kabisa hapa nchini katika mechi tatu za ligi kuu na moja ikizikutanisha zenyewe katika mchezo wa kirafiki wa Nani Mtani Jembe.

Refa (1) Jonesia Rukyaa alipochezesha mechi ya Mtani Jembe Decemba 2014 Uwanja wa Taifa.
Katika mechi za ligi alizozichezesha timu hizo, alifanikiwa kuiamua Simba katika michezo miwili ambapo mmoja iliibuka na ushindi na mwingine ikatoka sare. Mechi ya kwanza ilikuwa ni ya msimu wa 2014/15 dhidi ya Mtibwa Sugar, matokeo yalikuwa 1-1. Ya pili ikawa dhidi ya Coastal Union msimu huu katika Uwanja wa Taifa, Dar na kushinda kwa bao 1-0.
Yanga aliichezesha katika mechi moja kwenye Uwanja wa Taifa dhidi ya Mbeya City msimu huu, nayo ilishinda kwa mabao 3-0.
Katika Mtani Jembe ya mwaka 2014, Yanga ilitandikwa kwa mabao 2-0, kutokana na hali hiyo, Simba imefanikiwa kushinda michezo miwili na sare moja na Yanga ikashinda mmoja kati ya miwili ambayo mwamuzi alikuwa Rukyaa, ndiyo maana ya 2-1. Kwa hali hiyo, unaweza kusema Simba wamekuwa na bahati pale mechi inapoamuliwa na mwamuzi huyo kwa kushinda michezo yake miwili kati ya mitatu na Yanga ikiibuka na ushindi mchezo mmoja na kupoteza mmoja.

Hata hivyo, mechi hiyo ya Jumamosi hii baina ya wapinzani hao itakuwa ni ya pili kwake kuzichezesha Simba na Yanga baada ya ile ya Mtani Jembe ambayo aliwahi kukiri kuwa alikumbana na changamoto nyingi kutokana na ukubwa mechi hiyo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.