Thursday, February 18, 2016

Anonymous

AJALI Mbaya Yaua 50 Baada ya Basi Kugongana na Lori la Nyanya Uso Kwa Uso

Takriban watu 50 wamefariki dunia katika ajali mbaya ya barabarani kuwahi kutokea nchini humo katika kipindi cha miaka mingi.
Basi moja lililokuwa limejaa abiria liligongana uso kwa uso na lori lililokuwa limebeba nyanya huko kaskazini mwa nchi hiyo jana jioni.
 Rais wa Ghana, John Mahama ameielezea ajali hiyo kama ”habari mbaya” katika mtandao wake wa twitter na kuongeza kuwa huduma ya kukabiliana na masuala ya dharura inakabiliana na hali hiyo.
Baadhi ya walionusurika wamewaambia polisi kwamba breki za lori hilo zilifeli, lakini kiini cha ajali hiyo bado kinachunguzwa.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.