Sunday, November 1, 2015

Anonymous

[VIDEO] Miaka 12 Iiliyopita Siku Kama ya Leo Cristiano RONALDO Ndio Alifunga Goli Lake la Kwanza Akiwa na MAN United

Kila mmoja anamfahamu vizuri Cristiano Ronaldo ambaye anakipiga katika klabu ya Real Madrid ya Hispania na timu ya taifa ya Ureno. Ronaldo ambaye alijiunga na klabu ya Manchester United mwaka 2003 na kutimkia Real Madrid mwaka 2009 anaikumbuka kwa furaha siku kama ya leo akiwa na Man United. 

Cristiano Ronaldo anaikumbuka siku ya November 1 mwaka 2003 ndio ilikuwa mara yake ya kwanza kufunga goli akiwa na Man United, Ronaldo alifunga goli hilo kwa mpira wa faulo ambao ulitinga wavuni moja kwa moja na kuandika historia hiyo ambayo leo November 1 ni siku ya kumbukumbu yake. 

Goli hilo la Cristiano Ronaldo alifunga katika mechi dhidi ya Portsmouth goli ambalo lilianza kumpa heshima kutokana na namba ya jezi namba saba aliyokuwa anavaa ilikuwa imeachwa na mchezaji mahiri kipindi hicho David Beckham ambapo alitimkia Real Madrid staa huyo.
1411119211430_wps_49_MANCHESTER_ENGLAND_APRIL_
Hii ni video ya goli la kwanza la Cristiano Ronaldo akiwa na Man United goli ambalo alilifunga November 1 2003.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.