Sunday, November 1, 2015

Anonymous

MATOKEO ya Mechi Zote za Ligi Kuu Tanzania Bara Leo Jumapili...AZAM Yaishusha YANGA SC Kileleni!

Katika Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Azam FC imefanikiwa kileleni mwa msimamo baada ya kuibugiza Toto Africans ya Mwanza magoli 5-0 yaliyofungwa na Shomari Kapombe (2) Didier Kavumbagu (2) na Kipre Tchetche. 

Huko Tanga wanakimanumanu African Sports wamekubali kichapo cha magoli 2-0 toka kwa JKT Ruvu wakati huko Mbeya, wenyeji Tanzania Prisons wamelazimishwa sare ya 2-2 na Ndanda FC ya Mtwara. Kwa habari hizo na nyinginezo usikose kuangalia kipindi cha Mshikemshike cha Azam Tv kuanzia saa 2.30 usiku huu.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.