Chama
 cha mapinduzi (CCM) kimeibuka kidedea katika uchaguzi wa ubunge Jimbo 
la Ulanga baada ya mgombea wake, Goodluck Mlinga kupata kura 25,902 sawa
 na asilimia 69.78 akiwashinda wapinzani wake katika uchaguzi 
uliofanyika jana wilayani Ulanga mkoa wa Morogoro.
Akitangaza
 matokeo ya uchaguzi huo katika Ukumbi wa Halmashauri ya wilaya ya 
Ulanga usiku wa kuamkia leo, Isabela Chilumba alimtangaza mgombea wa 
CCM, Goodluck Mlinga kuwa ndiye mshindi wa kiti hicho baada ya kuwabwaga
 wenzake wa chama cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) na ACT-Wazalendo.
Mgombea
 wa CHADEMA Pancras Michael Ikongoli alipata kura 10,592 sawa na 
asilimia 28.53 wakati mgombea kupitia ACT-Wazalendo yeye akipata kura 
6,26 sawa na asilimia 1.69
Uchaguzi
 huo umefanyika Novemba 22 ikijumuisha vituo vya kupigia kura 203 katika
 kata 21 huku kukiwa na idadi ya wapigakura 76,715 waliojiandikisha 
katika daftari la kudumu la wapigakura.
Jumla ya wapigakura 37,499 walijitokeza kupiga kura huku kura 379 zikiharibika wakati kura halali zikiwa 37,120.
Kwa
 upande wa mgombea wa CCM, Goodluck Mlinga aliwashukuru wananchi wa 
jimbo la Ulanga kwa kumchagua kuwa mbunge wao na kuahidi kuitumikia kazi
 hiyo kwa moyo mmoja na kuomba ushirikiano kutoka kada mbalimbali ili 
kutekeleza majukumu yake hayo mapya.

 

 
 
 
 
Note: Only a member of this blog may post a comment.