Wakati Bunge la Kumi na Moja likitarajiwa kuanza vikao vyake wiki ijayo mjini Dodoma, Samuel Sitta na Anne Makinda, waliokalia kiti cha Spika wa mabunge mawili yaliyopita, wanatajwa kuwamo kwenye mchuano mwingine wa kuwania nafasi hiyo ya kuongoza chombo hicho cha kutunga sheria.
Majina ya makada hao wawili wa CCM, ambao mwaka huu hawakugombea ubunge kwenye majimbo yao, ni miongoni mwa watu kadhaa wanaotajwa kuwania kuongoza Bunge la 11 ambalo linatarajiwa kuanza vikao vyake wiki ijayo.
Kada mwingine wa CCM ambaye amekuwa akitajwa kwa muda mrefu ni mbunge wa Ilala, Mussa Hassan Zungu ambaye anatarajiwa kutoa upinzani mkubwa kwa wawili hao endapo ataingia kwenye mchakato wa kuwania nafasi hiyo.
Wengine wanaotajwa kuitaka nafasi hiyo ni mbunge mteule wa Peramiho, Jenister Mhagama, mbunge mteule wa Kibakwe, George Simbachawene na Job Ndugai ambaye ni Naibu Spika wa Bunge lililomaliza muda wake.
Kiti cha spika kinaweza kuwaniwa na mtu yeyote ambaye atapitishwa na chama chake bila ya kujali kama ni mbunge. CCM hutoa fursa kwa wanachama wake kuomba nafasi hiyo na baadaye kikao cha wabunge wa chama hicho hukutana kupitisha jina la mgombea mmoja.
Iwapo mgombea hatakuwa mbunge mteule, ni lazima jina lake lipitishwe na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Iwapo wawili hao wataingia kwenye kinyang’anyiro hicho, Sitta, aliyeongoza Bunge la Tisa ambalo linasifika kwa kuruhusu hoja zilizoibana Serikali, na Makinda, aliyeongoza Bunge la Kumi lililoibua kashfa zilizolazimisha mawaziri kujiuzulu, watakuwa wakipambana kwa mara ya pili baada ya kukutana mwaka 2010 wakati CCM ilipomtosa Sitta kwa hoja ya “kutaka Spika mwanamke”.
Habari kutoka kwa watu walio karibu naye zinasema Sitta, ambaye ni Waziri wa Uchukuzi, atapeleka jina lake CCM kwa ajili ya kuteuliwa kuwania nafasi hiyo.
Taarifa hizo zilithibitishwa na msemaji wa mbunge huyo wa zamani wa Urambo Mashariki, John Dotto ambaye alilieleza gazeti hili kuwa Sitta atawania nafasi hiyo kutokana na uwezo na uzoefu alionao wa kuendesha Bunge. Alisema Sitta anaamini kuwa uwezo wake aliouonyesha katika kuendesha Bunge la Tisa (2005 hadi 2010) akitumia kaulimbiu yake ya “Spika wa Kasi na Viwango”, utamfanya aendane na kasi ya utendaji wa Rais Mteule, Dk John Magufuli.
Habari zaidi zinaeleza kuwa Sitta ana nafasi kubwa ya kuibuka mshindi kutokana na rekodi yake na pia kukubalika na wabunge wengi wa CCM na hata wa vyama vya upinzani.
Hata hivyo, Sitta hakupatikana kueleza kiundani kuhusu suala hilo kutokana na kuwa nje ya nchi. Alitarajiwa kurejea jana jioni.
Baada ya kuongoza Bunge lililomlazimisha Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kujiuzulu, Sitta alijaribu kutetea nafasi yake mwaka 2010, lakini akagonga mwamba. Baadhi ya watu walimuona kuwa ni mtu aliyekuwa akiruhusu mijadala ya kuibana Serikali, kitu kilichofanya ajijengee uadui na baadhi ya vigogo.
Kwa upande wa Zungu, ambaye alikuwa mmoja wa wenyeviti wa Bunge la Kumi, hakutaka kukanusha wala kuthibitisha suala hilo alipoulizwa na gazeti hili.
Zungu aliliambia gazeti hili jana kuwa chama chake bado hakijatoa mwongozoo wowote hadi kufikia jana jioni na hivyo hawezi kuzungumzia suala hilo.
Mtu mwingine anayetajwa kwenye kinyang’anyiro hicho ni Naibu Spika anayemaliza muda wake, Job Ndugai, ambaye pia hakutaka kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa bado anauguza ‘majeraha’ ya Uchaguzi Mkuu.
Ndugai, ambaye amerudi bungeni akiliwakilisha Jimbo la Kongwa, alisema wiki hii atavieleza vyombo vya habari kama atawania nafasi hiyo.
Jibu kama hilo lilitolewa na Mhagama, ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Bunge la Kumi kabla ya kuteuliwa kuwa waziri. Mbunge huyo wa Peramiho alisema hawezi kuzungumzia vyema suala hilo kwa sababu yupo katika matayarisho ya hafla fupi ya kuapishwa kwa Rais Mteule.
Majina ya makada hao wawili wa CCM, ambao mwaka huu hawakugombea ubunge kwenye majimbo yao, ni miongoni mwa watu kadhaa wanaotajwa kuwania kuongoza Bunge la 11 ambalo linatarajiwa kuanza vikao vyake wiki ijayo.
Kada mwingine wa CCM ambaye amekuwa akitajwa kwa muda mrefu ni mbunge wa Ilala, Mussa Hassan Zungu ambaye anatarajiwa kutoa upinzani mkubwa kwa wawili hao endapo ataingia kwenye mchakato wa kuwania nafasi hiyo.
Wengine wanaotajwa kuitaka nafasi hiyo ni mbunge mteule wa Peramiho, Jenister Mhagama, mbunge mteule wa Kibakwe, George Simbachawene na Job Ndugai ambaye ni Naibu Spika wa Bunge lililomaliza muda wake.
Kiti cha spika kinaweza kuwaniwa na mtu yeyote ambaye atapitishwa na chama chake bila ya kujali kama ni mbunge. CCM hutoa fursa kwa wanachama wake kuomba nafasi hiyo na baadaye kikao cha wabunge wa chama hicho hukutana kupitisha jina la mgombea mmoja.
Iwapo mgombea hatakuwa mbunge mteule, ni lazima jina lake lipitishwe na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC).
Iwapo wawili hao wataingia kwenye kinyang’anyiro hicho, Sitta, aliyeongoza Bunge la Tisa ambalo linasifika kwa kuruhusu hoja zilizoibana Serikali, na Makinda, aliyeongoza Bunge la Kumi lililoibua kashfa zilizolazimisha mawaziri kujiuzulu, watakuwa wakipambana kwa mara ya pili baada ya kukutana mwaka 2010 wakati CCM ilipomtosa Sitta kwa hoja ya “kutaka Spika mwanamke”.
Habari kutoka kwa watu walio karibu naye zinasema Sitta, ambaye ni Waziri wa Uchukuzi, atapeleka jina lake CCM kwa ajili ya kuteuliwa kuwania nafasi hiyo.
Taarifa hizo zilithibitishwa na msemaji wa mbunge huyo wa zamani wa Urambo Mashariki, John Dotto ambaye alilieleza gazeti hili kuwa Sitta atawania nafasi hiyo kutokana na uwezo na uzoefu alionao wa kuendesha Bunge. Alisema Sitta anaamini kuwa uwezo wake aliouonyesha katika kuendesha Bunge la Tisa (2005 hadi 2010) akitumia kaulimbiu yake ya “Spika wa Kasi na Viwango”, utamfanya aendane na kasi ya utendaji wa Rais Mteule, Dk John Magufuli.
Hata hivyo, Sitta hakupatikana kueleza kiundani kuhusu suala hilo kutokana na kuwa nje ya nchi. Alitarajiwa kurejea jana jioni.
Baada ya kuongoza Bunge lililomlazimisha Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kujiuzulu, Sitta alijaribu kutetea nafasi yake mwaka 2010, lakini akagonga mwamba. Baadhi ya watu walimuona kuwa ni mtu aliyekuwa akiruhusu mijadala ya kuibana Serikali, kitu kilichofanya ajijengee uadui na baadhi ya vigogo.
Kwa upande wa Zungu, ambaye alikuwa mmoja wa wenyeviti wa Bunge la Kumi, hakutaka kukanusha wala kuthibitisha suala hilo alipoulizwa na gazeti hili.
Zungu aliliambia gazeti hili jana kuwa chama chake bado hakijatoa mwongozoo wowote hadi kufikia jana jioni na hivyo hawezi kuzungumzia suala hilo.
Mtu mwingine anayetajwa kwenye kinyang’anyiro hicho ni Naibu Spika anayemaliza muda wake, Job Ndugai, ambaye pia hakutaka kuzungumzia suala hilo kwa madai kuwa bado anauguza ‘majeraha’ ya Uchaguzi Mkuu.
Ndugai, ambaye amerudi bungeni akiliwakilisha Jimbo la Kongwa, alisema wiki hii atavieleza vyombo vya habari kama atawania nafasi hiyo.
Jibu kama hilo lilitolewa na Mhagama, ambaye pia alikuwa mwenyekiti wa Bunge la Kumi kabla ya kuteuliwa kuwa waziri. Mbunge huyo wa Peramiho alisema hawezi kuzungumzia vyema suala hilo kwa sababu yupo katika matayarisho ya hafla fupi ya kuapishwa kwa Rais Mteule.


Note: Only a member of this blog may post a comment.