Saturday, November 28, 2015

Anonymous

Baada ya Utunzaji wa Kumbukumbu Zake Kwa Tattoo, Zlatan IBRAHIMOVIC Kaja na Hii ya Utunzaji wa Magoli Yake [+VIDEO]

Ni headlines za staa wa soka anayeipeperusha vyema bendera ya Sweden na anakipiga katika klabu ya Paris Saint Germain ya Ufaransa Zlatan Ibrahimovic, ameingia katika headlines kadhaa mwaka 2015 ikiwemo kushinda tuzo ya mchezaji bora wa Sweden kwa mara ya tisa mfululizo na mara 10 kwa jumla.
2EDAD23F00000578-3336267-Zlatan_Ibrahimovic_has_launched_a_website_called_Zhowtime_with_v-a-4_1448625914536
November 27 mkali huyo wa Sweden ametangaza kuanzisha mtandao maalum ambao utakuwa unawekwa video na taarifa za magoli yake katika historia yake ya soka toka yupo Malmo, Ajax na vilabu vingine pamoja na magoli yake aliyoshinda akiwa na timu yake ya taifa ya Sweden. Mtandao wa Zlatan unaitwa “Zhowtime” jina ambalo limetungwa na waandishi wa habari wa Sweden.
2EDAD27300000578-3336267-The_website_features_YouTube_clips_of_the_majority_of_Zlatan_s_g-a-6_1448626003107
Huu ni muonekano wa mtandao huo wa Zhowtime
Watafiti wa Zlatan wametumia mwaka mzima kuandaa na kutafuta magoli ya staa huyo ambayo utakuwa unaweza kutafuta kwa msimu na Ligi, katika mtandao huo utapata kuona magoli zaidi ya 300 aliyofunga kwa ngazi ya klabu na zaidi ya 50 kwa timu yake ya taifa ya Sweden, huu ni utaratibu mwingine wa staa huyo wa kutunza kumbukumbu zake baada ya kuzoea kumuona akitumia mwili wake kama sehemu ya kutunza kumbukumbu zake muhimu kwa michoro ya tattoo.
Video ya moja kati ya magoli makali ya Zlatan Ibrahimovic

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.