Wabunge hao awali walitoa msimamo wao wa kutokubali Dk Ali Shein kuhudhuria Bunge hilo wakati rais atakapoingia Bungeni kulihutubia Bunge kwa kuwa hawamtambui kama rais wa Zanzibar kwani kwa mujibu wa Katiba muda wake umekwisha.
Kelele za zomeazomea ziliibuka ghafla wakati Rais Dk Shein alipoingia bungeni hali iliyoondoa utulivu wa Bunge.
Hata hivyo, Mbunge pekee wa upinzani, Zitto Kabwe (ACT – Wazalendo) alibaki ndani ya Bunge kwa utulivu na kuendelea kusikiliza hotuba ya Rais.
Awali, wabunge hao walimuandikia barua Spika wa Bunge wakihoji uhalali wa hotuba ya Rais bungeni endapo Dk Shein atahudhuria Bunge hilo kama Rais wa Zanzibar.
Ukawa wameendelea kushinikiza Tume ya Taifa ya Uchaguzi ya Zanzibar (NEC) kumtangaza mshindi wa nafasi ya Urais wa Zanzibar, huku mgombea wa CUF Maalim Seif Sharif Hamadi akidai kuwa ameshinda kutokana na kura halali alizokusanya kwenye vituo vyote.
Baada ya kuombwa mara tatu na Spika wa Bunge, wabunge kutoka vyama vya upinzani waamuriwa kutoka nje ya Bunge kutokana na kuanzisha mzozo Na tafaruku punde tu alipotambulishwa Dr Shein kama Rais wa Zanzibar.Kutoka Bungeni Live #azamTWO fuatilia Rais Magufuli akihutubia Bunge la 11.
Posted by Azam TV on Friday, November 20, 2015
DR. ALI MOHAMED SHEIN APOKEWA NA ZOMEA ZOMEA KUTOKA KWA WABUNGE WA UPINZANI WAKATI WA UZINDUZI WA BUNGE LA KUMI NA MOJAMustakabali wa wa demokrasia Tanzania bado ni kitendawili kufuatia Tume ya Uchaguzi Zanzibar kutoa tamko la kufuta uchaguzi wa Zanzibar.#HABARI Aliyeingia hivi sasa Bungeni katika uzinduizi wa Bunge ni Rais wa Zanzibar Dkt Ali Mohamed Shein,kelele nyingi zinasikika kutoka kwa wabunge wa UKAWA wakipinga kutomtambua huku wakilitaja jina la Maalim SeifKelele za wabunge zinaimba "Maalif Seif, Maalim Seif, Maalim Seif, Maalim Seifu..." Lakini taratibu zinaendeleaSpika wa Bunge Job Ndugai amewaamuru wabunge wanaopiga kelele watoke nje. Askari wameingia na kuwaamuru wabunge watoke nje, wabunge wote waliokuwa wakipiga kelele wametoka njeQuote : Magufuli...nitashirikiana na viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na hasa viongozi wa vyama vya CCM na CUF kuhakikisha hali iliyopo sasa Zanzibar inapatiwa muafaka kwa haraka..... - Dk. John Pombe Magufuli, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania #BungeniDodoma.
Posted by Zanzibar Post on Friday, November 20, 2015
Note: Only a member of this blog may post a comment.