Rais Jakaya Kikwete.
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt Jakaya Mrisho Kikwete amefanya uteuzi katika Mahakama kama ifuatavyo;
Rais amemteua Bi. Katarina Revocati kuwa Msajili Mkuu wa Mahakama ya
Tanzania (Chief Registrar). Kabla ya uteuzi huu, Bi. Revocati alikuwa
Msajili wa Mahakama ya Rufani.
Rais pia amemteua Ndugu John Rugalema Kahyoza kuwa Msajili wa
Mahakama ya Rufani na kabla ya uteuzi huu, Ndugu Kahyoza alikuwa Msajili
wa Mahakama Kuu.
Mwingine aliyeteuliwa ni Ndugu Ilvin Claud Mugeta ambaye anakuwa Msajili wa Mahakama Kuu. Kabla
ya Uteuzi huu ndugu Mugeta alikuwa Mkurugenzi wa Ukaguzi na Maadili.
ya Uteuzi huu ndugu Mugeta alikuwa Mkurugenzi wa Ukaguzi na Maadili.
Uteuzi huu umeanza tarehe 3 Oktoba, 2015.
Imetolewa na:
Premi Kibanga,
Mwandishi wa Habari wa Rais,
Msaidizi
Ikulu,
DAR ES SALAAM.
19 Oktoba, 2015.

Note: Only a member of this blog may post a comment.