Collabo ya
mwisho ya Diamond Platnumz na msanii wa Kenya ni ile aliyoshirikishwa na
Victoria Kimani kwenye wimbo Prokoto alikuwemo Ommy Dimpoz pia.
Baada ya hapo,
Diamond amekuwa akifanya ngoma na wasanii wa Nigeria, Afrika Kusini na
Marekani zaidi. Hata collabo na wasanii wenzake wa Bongo zimekuwa za
nadra pia na hivyo kumfanya kuendelea kuwa msanii anayetafutwa zaidi kwa
collabo Afrika Mashariki.
Lakini kuna
msanii wa Kenya aliyepata nafasi ya kumshirikisha staa huyo na huyo si
mwingine zaidi ya Esther Akoth maarufu kwa jina la Akothee.
Muimbaji huyo
amekuja nchini kurekodi wimbo huo na Diamond kwenye studio zake za
Wasafi Classic, WCB. Wawili hao waliingia kwenye studio usiku wa kuamkia
Alhamis hii.
Hiyo inakuwa
collabo ya pili kubwa kwa Akothee kuifanya mwaka huu baada ya hivi
karibuni kurekodi wimbo na Flavour wa nchini Nigeria.
Hivi karibuni aliachia video ya wimbo wake ‘Shengerera Mama’ iliyoongozwa na God Father.

Note: Only a member of this blog may post a comment.