Sunday, October 25, 2015

Anonymous

NEWS UPDATES: Kuhusu Mgombea Urais TLP Kushindwa Kupiga Kura

LIMOOOOOOOOOO
Mgombea urais kwa tiketi ya Tanzania Labour Party (TLP), Maximillian Lyimo.

Kama kandiliyetu.com tulivyowaahidi mapema leo asubuhi kuwa tutawaletea taarifa kamili kuhusu suala hili. Hii hapa tumekuwekea mdau...endelea!
Mgombea urais kwa tiketi ya Tanzania Labour Party (TLP), Maximillian Lyimo ameshindwa kupiga kura leo katika Kituo cha Njia Panda Jimbo la Vunjo mkoani Kilimanjaro baada ya kukosekana taarifa zake kituoni hapo.
Lyimo aliyejiandikishia mkoani Dar es Salaam, jana alienda kufunga kampeni zake Jimbo la Vunjo na kulala huko, asubuhi ya leo alienda kituo cha Njia Panda jimboni humo ili akapige kura. 

Baada ya kufika kituoni hapo akiwa na kitambulisho chake cha kupigia kura, alizuiwa baada ya kukosekana fomu namba 19 ambayo kisheria inamuwezesha mgombea urais kupiga kura ya kumchagua rais kwenye kituo chochote hivyo akakoswa fursa ya kupiga kura.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.