Wednesday, October 28, 2015

Anonymous

NEC Yajibu Malalamiko ya UKAWA

Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, Jaji Damian Lubuva amejibu malalamiko yaliyotolewa na viongozi wa vyama vya upinzani vinavyounda Ukawa, kuhusu utofauti kati ya baadhi ya matokeo yanayotangazwa na Tume hiyo na yale yaliyokuwepo vituoni.

Akiongea hivi punde kabla ya kuanza kutangaza matokeo mengine ya majimbo 54, Jaji Lubuva amekanusha taarifa zilizotolewa jana na viongozi wa Ukawa na kutolea ufafanuzi matokeo ya nafasi ya urais yanayopokelewa na kutangazwa na Tume hiyo. 
Hivi ndivyo alivyoeleza:
“Tusingependa wakati huu kulumbana na vyama vya siasa au wadau wengine. Hiyo ndiyo nia yetu. Lakini pale panapokuwa na upotoshaji wa hali ya juu, Tume inalazimika kusema machache. 

"Moja ni upotoshaji unandelea sasa hivi kwamba Tume ya Uchaguzi, matokeo tunayosoma hapa yamechakachuliwa kuhusu wagombea wa urais.  

"Hiyo sio kweli hata kidogo, ningependa kutumia nafasi hii kupitia ninyi waandishi wa habari kuelewesha wananchi kwamba wasipotoshwe.

“Nilishawahi kusema kwamba tunachofanya sisi hapa ni kusoma na tumeshahakiki yale ambayo yametokea katika majimbo, hayo ndiyo yaliyokuwa yamehakikiwa wakiwemo mawakala wa vyama mbalimbali.  

Updates:
Lowassa  anategemea  kuongea  tena na  vyombo  vya  habari muda  wowote  mchana  huu.

Endelea kufuatilia hapa kandiliyetu.com kwa updates zote muhimu za uchaguzi mkuu na matukio mbalimbali kama bado hauja-like page yetu ya facebook bonyeza hapa 

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.