Friday, October 16, 2015

Anonymous

JOSE MOURINHO Kapigwa Stop Moja…Halafu na Milioni 160 Zinamtoka

Chama cha soka England (FA) kimempa kocha wa Chelsea Jose Mourinho adhabu kutokana na utovu wa nidhamu ambapo anatakiwa kulipa faini ya dola 77,000 ambazo kibongobongo ni zaidi ya milioni 160 pamoja na kufungiwa mechi moja huku FA wakiangalia mwenendo wake. 
Meneja huyu wa Chelsea alimshambulia kwa maneno mwamuzi Robert Madley aliyechezesha mechi ya Chelsea vs Southampton iliyomalizika kwa 1- 3 na ikamfanya Mourinho akasirishwe na Refa Madley kutoipa timu yake penati na kudai Waamuzi wanaogopa kutoa uamuzi kwa timu yake.
Hii kauli ndio ikawafanya FA wamfungulie Mashitaka ya utovu wa nidhamu wakidai kauli za Mourinho zinazochochea vurugu.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.