Majina mawili ya Mgombea urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi
(CCM), Dk. John Pombe Joseph Magufuli yana historia yake ya jinsi
yalivyopatikana. Majina hayo mawili ‘Pombe’ na ‘Magufuli’ yalitokana na
bibi na babu wazaa baba yake Magufuli.
Jina la ‘Pombe’ alipewa na bibi yake kwani wakati anazaliwa bibi yake
alikuwa amepika pombe siku hiyo na jina la ‘Magufuli’ lilitokana na
babu yake ambaye alikuwa shujaa wa kucheza ngoma za asili aliyepewa jina
Magufuli kwani kila alipokuwa akicheza ngoma alikuwa anawashinda
wengine hivyo kitendo hicho kilifananishwa na kufuli linavyofungwa
mlangoni.

Note: Only a member of this blog may post a comment.