Thursday, October 22, 2015

Anonymous

FURSA: Je, Unataka kwenda Kuishi Kufanya Kazi Marekani? Nafasi Hii ni Yako

Hauitajika kulipa hata senti tano ni buree! Jaribu bahati yako, muda uliobakia ni mchache sana. Mwisho wa kutuma maombi ni November 3, 2015.

 
Kila mwaka Serikali ya Marekani kupitia Ubalozi wa Marekani imekuwa ikitoa nafasi ya kutuma maombi ya watu kwenda kuishi Marekani kupitia mpango ujulikano kama “Diversity Visa program (DV-2017)”. Ni kama vile bahati nasibu na hapa  hautakiwi kutoa au kulipa chochote zaidi ya kuwa na picha yako ya digitali na kujaza maelezo machache kupitia mtandao wao wa  www.dvlottery.state.gov.
Nafasi hii inatolewa mara moja tu kwa mwaka na kwa mwaka huu dirisha la kutuma maombi liko wazi kuanzia Octoba 5, 2015 hadi Novemba 3, 2015.

Usikubali kutoa pesa kwa mtu au shirika lolote wanaokupata ahadi kuwa watakuongeza nafasi zaidi za wewe kushinda kuchaguliwa katika mpango huu. Unachotakiwa kufanya ni kuwa na internet na kutuma ombi mara moja tu kwa mwaka. Ukituma mara mbili au zaidi basi ombi lako litaenguliwa. Mamia ya watanzania wameshanufaika na mpango huu.
Angalizo: Maombi ni bure na usikubali kutapeliwa!
Kwa taarifa zaidi kwa lugha ya kiingereza bofya hapa http://1.usa.gov/1NRbPng.
Ukitaka kutuma mambi bofya hapa www.dvlottery.state.gov.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.