Ommy Dimpoz amesimulia namna alivyoingizwa mjini kwa kuibiwa simu
yake ya mkononi akiwa dukani jimboni Texas nchini Marekani alikokwenda
kwa ziara ya kimuziki.
Dimpoz ameliambia gazeti la Mtanzania kuwa baada ya kufanya show ya
kwanza aliamua kufanya ‘shopping’ kwenye duka moja kubwa la nguo mjini
Houston, lakini baada ya muda akajikuta hana simu.
“Niliangalia mfukoni sikuikuta, nikajaribu kuipiga haikuita
nilipomwambia mwenye duka akanipeleka katika kamera za usalama ndani ya
duka hilo nikamuona mwizi wa simu yangu alikuwa mmoja wa wateja katika
duka hilo,” alieleza Dimpoz.
Pia Ommy alisema simu hiyo ilikuwa na hifadhi ya nyimbo zake mpya
ambazo hakutarajia kuzitoa kwa sasa na vitu vingine binafsi vingi jambo
ambalo limemtia hasara kubwa.

Note: Only a member of this blog may post a comment.