Friday, September 11, 2015

Anonymous

KUFURU! Huu Ndio Mshahara Mpya wa Golikipa DAVID DE GEA Pale MNCHESTER UNITED!

Takribani siku 10 tangu uhamisho wake wa kwenda kujiunga na klabu ya Real Madrid kukwama, golikipa wa timu ya taifa ya Spain na klabu ya Manchester United, David De Gea ameamua kufanya uamuzi mwingine kuhusu hatma yake ndani ya klabu hiyo ya Uingereza.
David de Gea amesaini mkataba mpya wa kuendelea kubaki Manchester kwa miaka mengine minne baada ya mkataba wake wa sasa kuisha mwakani.
Golikipa huyo mwenye miaka 24 alianza mazungumzo ya mkataba mpya baada ya uhamisho wake ambao ungegharimu kiasi cha  Pound Mil. 29 kushindikana siku ya mwisho ya dirisha la usajili.
Hii ni #Tweet ya De Gea akitghibitisha kubakia Man United.
 
Mkataba mpya wa De Gea utamfanya kuwa golikipa anayelipwa zaidi kwa kulipwa mshahara usiopungua kiasi cha  Pound laki mbili kwa wiki.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.