Friday, September 11, 2015

Anonymous

Kocha Mzungu wa MAJIMAJI "Wanalizombe Atoa Mpya!

pic+kocha
Mohammed Mdose, Dar es Salaam
LICHA ya makocha wenzake kuziandaa timu na kujua ubora wake kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu Bara, hali ya mambo ni tofauti kwa Kocha Mkuu wa Majimaji, Mika Lonnstrom, raia wa Finland, ambaye mpaka sasa hajajua uimara wa kikosi chake, hivyo anataka kukijaribu kwenye mechi nne za mwanzo wa ligi.
Majimaji wataanza ligi kwenye uwanja wao wa Majimaji Songea kwa kucheza na JKT Ruvu, kisha Kagera Sugar halafu watawafuata Mgambo JKT, Uwanja wa Mkwakwani, Tanga, halafu Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro.

Akizungumza na Championi Ijumaa, kocha huyo aliyetua Majimaji miezi miwili iliyopita, alisema hakucheza mechi za kirafiki na timu kubwa ili kuipima timu yake kutokana na jinsi alivyoikuta ikiwa kwenye kiwango kidogo, hivyo alichokuwa akidili nacho ni kuijenga icheze kitimu.
“Kwa ugeni wetu huu katika ligi, lengo letu ni kubaki kwenye ligi na siyo kuwa mabingwa, nimefanya kazi kubwa ya kuijenga lakini sijajua imejengeka kwa kiasi gani. Nitaijaribu kwenye mechi nne za mwanzo wa ligi, kama bado nitaendelea kuzidi kuiimarisha,” alisema Lonnstrom.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.