Imelda Mtema
BAADA ya kupita ukimya mrefu bila kuzungumzia mapenzi, mrembo asiyepoteza ubora wake, Wema Sepetu ‘Madam’ amemtaja mwanaume anayetarajia kumzalia mtoto kuwa ni Luis Munana, raia wa Namibia.
Wema
alifunguka hayo juzikati mara baada ya mwandishi wetu kutaka kujua ana
mpango gani kwenye ulimwengu wa ‘malovee’ ndipo alipomwanika Luis kuwa
ndiye mwanaume pekee ambaye ameshafikia hatua ya kumuamini na yuko
tayari kuzaa naye kwa namna yoyote licha ya kujua ana tatizo la uzazi.
“Luis ndiyo kila kitu kwangu, ndiye mwanaume ambaye tunaelewana na
siyo mswahili kama kina mwafulani. Luis nitazaa naye hata kwa ku-adopt
(kuasili) mtoto kama njia za kawaida zitashindikana, ndiye mwanaume
ambaye nimepanga aje kuwa baba wa watoto wangu,” alisema Wema.
Kabla ya kufunguka hayo, Wema alikuwa akimposti mwanaume huyo ambaye alishiriki Shindano la Big Brother-Hotshorts (2014) kwenye ukurasa wake wa Instagram pasipo kuandika kama ni mpenzi wake lakini kwa sasa ameamua kuweka kila kitu hadharani.
Miezi kadhaa iliyopita, Wema aliwahi kuonekana na Luis katika pati ya Instagram iliyofanyika kwenye Viwanja vya Posta jijini Dar kisha wawili hao kudaiwa kulala pamoja katika hoteli moja jijini humo.
BAADA ya kupita ukimya mrefu bila kuzungumzia mapenzi, mrembo asiyepoteza ubora wake, Wema Sepetu ‘Madam’ amemtaja mwanaume anayetarajia kumzalia mtoto kuwa ni Luis Munana, raia wa Namibia.
Kabla ya kufunguka hayo, Wema alikuwa akimposti mwanaume huyo ambaye alishiriki Shindano la Big Brother-Hotshorts (2014) kwenye ukurasa wake wa Instagram pasipo kuandika kama ni mpenzi wake lakini kwa sasa ameamua kuweka kila kitu hadharani.
Miezi kadhaa iliyopita, Wema aliwahi kuonekana na Luis katika pati ya Instagram iliyofanyika kwenye Viwanja vya Posta jijini Dar kisha wawili hao kudaiwa kulala pamoja katika hoteli moja jijini humo.
Note: Only a member of this blog may post a comment.