Hamida HassanStaa wa
filamu na muziki, Sabrina Omary ‘Sabby Angel’ hivi karibuni amefunguka
siri iliyokuwa kwenye uvungu wa moyo wake kwamba analitamani sana penzi
la mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ ila anaumia kwa kuwa anajua
amechelewa.
Akichonga na Ijumaa hivi
karibuni, Sabby aliyewahi pia kuwa mpenzi wa Mwanamuziki Bob Junior
alisema anajuta kwa nini alichelewa kuzianika hisia zake kwani Diamond
ana sifa zote ambazo angependa mpenzi wake awe nazo.
“Yaani nimeficha hisia zangu siku nyingi
lakini bora niseme ukweli kwamba natamani kuwa na Diamond kimapenzi,
nahisi ni mwanaume anayejua kuishi na mwanawake,” alisema Sabby.

Note: Only a member of this blog may post a comment.