Kocha wa klabu ya Manchester City ya Uingereza Manuel Pellegrini
August 20 amekamilisha furaha yake ya kumsaini moja kati ya mabeki bora
anaowaamini na alikuwa akimuhitaji kwa muda sasa kabla ya August 20
kufanikiwa kumnasa nyota huyo wa Argentina aliyekuwa anaitumikia klabu ya Valencia ya Hispania Nicolas Otamendi.

Otamendi akisaini mkataba wa miaka mitano mbele ya Txiki Begiristain ambaye ni mkurugenzi wa michezo Man City
Otamendi akisaini mkataba wa miaka mitano mbele ya Txiki Begiristain ambaye ni mkurugenzi wa michezo Man City
Pound milioni 32 zilitosha kuishawishi klabu ya Valencia kumuachia nyota huyo ahamie Etihad kwa mkataba wa miaka mitano, Man City wamelipa kiasi hicho kwa ajili ya staa huyo aliyekuwa miongoni mwa wachezaji wanaounda kikosi bora cha Laliga katika msimu wa 2014-2015.
“Yupo imara ni mzuri katika mipira ya tackling na yupo vizuri kiufundi”>>> Manuel Pellegrini
Hizi ni picha baada ya kusaini Man City miaka mitano.

Note: Only a member of this blog may post a comment.