Saturday, August 15, 2015

Anonymous

MAWAZIRI HAWA WAWILI WA JK WAANGUKIA PUA KURA ZILIZORUDIWA ZA MAONI CCM

Mawaziri wawili wa Serikali ya Rais Jakaya Kikwete wameanguka kwenye marudio ya Kura za Maoni zilizofanyika juzi, huku matokeo ya Jimbo la Busega yakikwama baada ya Waziri wa Uvuvi na Maendeleo ya Mifugo, Dk. Titus Kamani kumshambulia msimamizi wa Uchaguzi. 

Walioanguka ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid (Rufiji) na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Mazingira), Dk. Binilith Mahenge (Makete), huku Dk Raphael Chegeni akiongoza kwenye Jimbo la Busega. 

Dk Kamani na wafuasi walizuia matokeo kutangazwa na kuibuka kwa vurugu zilizosababisha polisi kuingilia kati na kukamata watu wanne walioonekana kumuunga mkono.

Aliyeshinda ameshinda tu hakuna namna. Kilichofanywa na Waziri Kamani kumpiga msimamizi huyo ni mambo ya binadamu tu… lakini walioshindwa lazima wakubali matokeo na lazima yatangazwe,” alisema Paul Mzindakaya, Mkuu wa Wilaya ya Busega. 

Vurugu zilianza saa 4 asubuhi baada ya Dk Kamani, ambaye pia ni Mwenyekiti wa CCM wa Mkoa wa Simiyu, kuingilia kati wakati Mabiya, ambaye ni katibu wa Wilaya ya Meatu, akianza kutangaza matokeo. 

Baada ya Polisi waliokuwa na silaha kuimarisha ulinzi, Mabiya alisimama kutangaza matokeo lakini akakatishwa baada ya kurukiwa na watu walioonekana kumuunga mkono Waziri Kamani na kupigwa makonde mbele ya Polisi na Mzindakaya. 

Kipigo hicho kilimfanya Mabiya akimbilie ndani ya ofisi za chama hicho na kuacha askari wa Kikosi cha FFU wakitumia nguvu kudhibiti watu hao. 

Wakati wote wa vurugu hizo, Dk. Chegeni alikuwa amesimama pembeni mwa ofisi za chama hicho akishuhudia matukio hayo, lakini baadaye akaondoka akiwa amepanda gari lake huku akishangiliwa. 

Baada ya polisi kufanikiwa kutuliza ghasia, Mabiya alisimama tena kutangaza matokeo hayo, lakini Dk Kamani alimfuata na kumshambulia kwa makonde, kukazuka tafrani kubwa zaidi.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.