Saturday, August 15, 2015

Anonymous

Mapenzi ya WOLPER Kwa LOWASSA Usipime!

92d27__wolper2bongoclan.co_.tz_
MAPENZI! Staa wa sinema za Kibongo, Jacqueline Walper ‘Wolper’, amezidi kujipambanua mapenzi yake kwa mgombea urais kupitia Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa kwa kusema; “nampenda Lowassa hadi naumwa.”
lowassa2.jpg
Akizungumzia mapenzi yake hayo hivi karibuni, Wolper alibainisha kuwa Lowassa kwake ni zaidi ya rais hivyo ndiyo maana alikuwa akimnadi hadharani kupitia mitandao ya kijamii alipokuwa Chama cha Mapinduzi (CCM) na hata alipohamia Ukawa. 

“Nisiwe mnafiki, mimi nampenda Lowassa yeye kama yeye na si chama. Nimemuweka kwenye profile yangu katika simu, nikizima nikiwasha simu, namuona yeye. Huu ni uhuru wa kujieleza kila mtu anaweza kujieleza anavyotaka, namsapoti Lowassa kila atakapokuwepo,” alisema Wolper.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.