Gladness Mallya
REVENGE! Katika kile kinachoonekana kama kejeli kwa mke wake wa zamani aliyekorofishana naye, mtangazaji maarufu Gardner G. Habash, ametundika picha kwenye akaunti yake katika mtandao wa Instagram ikimuonyesha akiwa amempakata mwanamke mjamzito.
Katika maoni mbalimbali ya wadau waliozungumzia suala hilo, baadhi walimpongeza kwa kumpata mwanadada na kumpa ujauzito, huku wengine wakihoji kama huyo ndiye shemeji au wifi yao.
Wapo waliokwenda mbali zaidi na kudai mtangazaji huyo wa zamani wa Times FM, alikuwa amefanya kitendo hicho makusudi ili aweze kumkejeli Jide, ambaye alikaa naye kwa muda wa miaka kumi pasipo kupata mtoto.
“Jamani hivyo siyo vizuri maana anamkejeli tu dada yetu Jide, sijui anaona raha gani kumuumiza mwenzake moyo,” aliandika mdau mmoja.
“Yaa, ni kweli picha nimeweka mimi..lakini si kwa lengo la kumkejeli Jide, kwa nini nimkejeli? Mimi sina matatizo naye mbona, ni picha tu nimeweka..
“Huyo ni shemeji yangu, mke wa mdogo wangu mmoja kifamilia. Lakini usijali, wiki hii nitamwonyesha picha nzima ili watu wamtambue na nitawaeleza kwa kirefu,” alisema Gardner, ambaye pia ni mdau mkubwa wa muziki.
Wawili hao waliingia katika mtafaruku miezi kadhaa iliyopita na tangu wakati huo, hakuna hata mmoja kati yao aliyeweza kuzungumzia suala hilo moja kwa moja zaidi ya mafumbo wanayoyatoa kupitia akaunti zao katika mitandao ya kijamii. Jide hakupatikana kuzungumzia picha hiyo.
Note: Only a member of this blog may post a comment.