Tuesday, August 4, 2015

Anonymous

CHADEMA, UKAWA, Muacheni LOWASSA Aongoze Kampeni Yake

Uongozi CHADEMA, UKAWA, na wadau wa upinzani. Kama mmemualika Lowassa kusaidia kuiangusha C.C.M. basi ni kwa sababu ameonyesha dalili za mafanikio, na hiyo yote inatokana na mikakati yake ya siku nyingi pamoja na timu yake, ujumbe wake kwa umma, historia na mvuto wake kwa jamii.

Kama ndie yeye mnaetegemea kumpa abebe bendera basi muacheni Lowassa awe Lowassa, ikiwa ni pamoja na kumuacha ku control his message. Huu mpango wa Mwenyekiti na wasemaji wa chama kila asubuhi wanatoka na matamko kuhusu Dr. Slaa sijui Mnyika tuwaombee kwa Mungu sijui wamefanya lile na hili, wamesusa, hawajala, hawarudi nyumbani, that is extremely crippling to the Lowassa campaign. Mnamwondoa mgombea wenu kwenye national conversation badala ya kumuachia ukumbi.Mmeshampokea, mmeshampokea, hayo ni maji chini ya daraja.

Wengine wame focus kwenye "kwa nini havai gwanda," well, labda timu yake imeamua strategically kum project kama national leader, huwezi kwenda kwenye national election na magwanda ya chama kimoja. Kushinda uchaguzi Lowassa atahitaji kura za wapenda C.C.M. pia. Hii si kampeni ya CHADEMA, ni kampeni ya Lowassa, image ya CHADEMA is badly tainted right now, mwacheni mgombea ajinasibu kwa utashi wake mwenyewe. Kina Mbowe sogeeni pembeni kwa sasa tafadhalini, waacheni wakina Apson Mwang'onda wa run the campaign. Rai yangu kwa Lowassa, kwa sasa anzisha ofisi ya makao makuu ya kampeni mbali na Mtaa wa Ufipa. 

-JF

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.