Monday, July 20, 2015

Anonymous

YEMI ALADE Aonesha Mfano wa Kuigwa Kwa Alichowafanyia Kina VANESSA Mdee!

Licha ya kushindana yanapokuja maswala ya Tuzo, lakini kumekuwepo na tatizo la kugeuza matokeo kuwa chuki kwa baadhi ya wasanii, kitu ambacho msanii wa Nigeria Yemi Alade alifanya kinyume chake siku ya tuzo za 2015 MTV MAMA.
yemi
Yemi Alade ndiye mshindi wa kipengele cha ‘Best Female’ alichokuwa anawania pia Vanessa Mdee.
Wakati wa kwenda kupokea tuzo hiyo Yemi aliwachukua wasanii aliokuwa akichuana nao kwenye kipengele hicho, ambao ni Vanessa Mdee (Tanzania) , Seyi Shay (Nigeria), Bucie (South Africa) na Busiswa (South Africa) na kwenda nao jukwaani kuashiria upendo na umoja licha ya yeye kuibuka mshindi.

Kupitia ukurasa wake wa Insta Yemi aliandika kile kilichojiri baada ya jina lake kutajwa kuwa ndiye mshindi:
“Meneja wangu aliniambia simama kama mara tatu, ni kama nililisahau jina langu mwenyewe…halafu mentors wangu Peter na Paul Okoye wakanikumbusha natakiwa niende kupokea tuzo yangu…Lmaooo.. Isingewezekana kuwasahau dada zangu Seyi Shay, Vanessa Mdee, Bucie na Busiswa, sisi ni nguvu moja, tunaenda pamoja.”
Kwenye post nyingine aliandika:
“I didn’t write a speech…”didn’t hezperetit” lol but everything that came out from my mouth was to the glory of God alone….. Dedicatedtotheteamthatneversleeps.#effyzziebaby ..#stronggirls and # Mytangerines.”

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.