Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania,
Saimon Mwakifwamba amefungua kinywa chake na kusema kuwa mwaka huu
lazima aachie ngazi ili awapishe wengine waendeleze gurudumu.
Akizungumza na gazeti hili juzi mjini
hapa, Mwakifwamba alisema kuwa muda aliokaa madarakani unatosha hivyo ni
vyema akawapisha wengine wenye vigezo vya kuongoza.
“Watu wengi wanajua mimi sipendi kuachia
ngazi, siyo kweli kabisa! Mwaka huu naachia ngazi ili mwingine aweze
kuchukua kijiti. Najua wapo wenye nia thabiti ya kukuza tasnia yetu,
nitawapisha,” alisema Mwakifwamba.

Note: Only a member of this blog may post a comment.