VIJANA
waendesha bodaboda walizua mtafaruku wa aina yake baada kujikusanya na
kutaka kuichoma moto daladala yenye namba za usajili T 219 BSJ
inayofanya safari zake kati ya Mjini na Bingwa, mkoani Morogoro ambayo
ilisababisha ajali iliyomhusisha dereva bodaboda mwenzao aliyefahamika
kwa jina moja la Steve.
Tukio hilo lililozua taharuki ya aina
yake miongoni mwa abiria, lilitokea juzikati maeneo ya njia panda ya
Chuo Cha Ualimu cha Kigurunyembe ambapo kwa mujibu wa mashuhuda, dereva
wa daladala aliyefahamika kwa jina la Hamad Rashid ‘alimuovateki’
bodaboda kisha kusimama ghafla ndipo bodaboda alipoligonga daladala kwa
nyuma.
“Huyu dereva wa daladala alimuovateki
bodaboda sasa ghafla akaona abiria, akasimama na kusababisha bodaboda
amvae kwa nyuma,” alisema shuhuda mmoja.
Shuhuda huyo alizidi kueleza kuwa, baada
ya bodaboda huyo kuligonga daladala kwa nyuma, dereva wa daladala
alitimua mbio baada ya kuona vijana wa bodaboda wanakusanyika eneo hilo.
“Baadaye dereva wa daladala alirejea
baada kuona polisi wamefika eneo hilo ambapo aliwaambia kuwa dereva huyo
wa bodaboda ndiye aliyesababisha kauli ambayo haikuwa kweli,”
alimalizia shuhuda huyo.
Hadi mwandishi wetu anaondoka eneo hilo,
aliwaacha askari wa usalama barabarani wakichukua maelezo kwa dereva wa
daladala kwa ajili ya taratibu za kisheria huku dereva wa bodaboda
ambaye alipata majeraha akipelekwa Hospitali ya Morogoro kwa ajili ya
matibabu.

Note: Only a member of this blog may post a comment.