TUZO za KTMA zilitolewa Jumamosi iliyopita Mlimani
City na kushuhudia msanii Ali Kiba akiondoka na tuzo tano peke
yake.Jumla ya tuzo 26 zilitolewa usiku huo. Ukiachana na hiyo lakini pia
kikubwa kilichotizamwa na wadau wengi waliojitokeza ni ishu ya mavazi.
Wengine
walioonekana kutokelezea ni Mwana FA, Prof Jay na Kundi la Weusi hao
wote walikuwa ndani ya suti za mikono mirefu. Wapenzi wa muda mrefu
prodyuza, Nahreel na Aika nao walikuwa na mavazi yao yaliyowatoa
‘mwake’.
Aliojaribu kuvaa kama wasanii wa mamtoni na kuondoa utamaduni wa
Kiafrika ni; Msanii Bora wa Kike, Vanessa Mdee ambaye anafanya vizuri
kimataifa kwa sasa kwa upande wa wadada alivaa nguo ambazo ziliacha
kifua chake wazi sehemu kubwa.
Faiza Ally alitoa mpya baada ya kushona nguo ya kitenge vipandevipande na kusababisha kuacha wazi eneo kubwa la mwili wake sambamba na ‘makalio’ kuonekana wazi licha ya kutinga na chupi ya kitenge. Wengine ni Queen Darleen na Linah Sanga nao walitupia nusunusu.
Baadhi ya walioonekana kuvutia wadau wengi
waliokuwemo ukumbini hapo na hata wale waliokuwa wakitazama kupitia
runinga.Muigizaji Wema Sepetu aliyekuwa na meneja wake, Martin Kadinda,
walivutia wadau kwa kiasi kikubwa kwa namna walivyo vaa halikadhalika na
Jokate Mwegelo.
Licha ya kutozoeleka kuonekana akiwa katinga gauni, kwa mara ya
kwanza kwenye tuzo za KTMA 2014/15, Fetty ambaye ni mtangazaji wa
Clouds Radio alitupia gauni la bluu bahari wakati akiongoza shoo ‘host’
sambamba na Zembwela aliyekuwa ndani ya suti, mwingine ni mtanashati
Perfect Crispin wa Clouds FM.Faiza Ally alitoa mpya baada ya kushona nguo ya kitenge vipandevipande na kusababisha kuacha wazi eneo kubwa la mwili wake sambamba na ‘makalio’ kuonekana wazi licha ya kutinga na chupi ya kitenge. Wengine ni Queen Darleen na Linah Sanga nao walitupia nusunusu.

Note: Only a member of this blog may post a comment.