Monday, June 22, 2015

Anonymous

LIVE! KCEE ANASWA SOKONI AKINUNUA MAFUTA YA MAWESE!

STAA wa 'Limpopo', Kcee akiwa kwenye soko kuukuu akinunua mafuta ya mawese pamoja na matunda.
LAGOS, Nigeria
STAA wa 'Limpopo', Kcee wikiendi iliyopita alituma picha kwenye ukurasa wake wa Instagram akiwa sokoni.
 Kcee siyo mgeni kwa wadau wa muziki wa Bongo, kwani ameshafanya ngoma na Shetta inayoitwa Shikorobo lakini pia amemshirikisha Diamond Platinumz  katika wimbo mpya wa ‘Love Boat’.
 Kcee alituma picha hiyo akionekana akiwa kwenye soko kuukuu akinunua mafuta ya mawese pamoja na matunda huku baadhi ya wauzaji na wanunuzi waliokuwepo eneo hilo wakimshangaa.
Baada ya kupost picha hiyo, mashabiki waliofanikiwa kuiona walimpongeza kwani ni ngumu sana kwa msanii kuonekana akiwa kwenye soko ‘lililochoka’ akinunua vitu.
Lucy Mgina na mtandao

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.