Ijumaa ya April 24 nakukaribisha tena mtu wangu POWERBREAKFAST ya Clouds FM imefanya uchambuzi wa story zote kubwa kwenye kurasa za Magazeti TZ leo..
Ugonjwa wa macho mekundu umeibuka katika
maeneo mbalimbali Dar, NEC imetangaza zabuni ya ununuzi wa vifaa
vitakavyotuka kupigia kura, Polisi Bariadi wamesema kuwa kada wa CCM
Ahmed Ismail ndio alirusha risasi ili kuwatawanya watu waliokuwa
wameziba njia, Mbunge Augustino Mrema amesema
ni ndoto kwa vyama vya upinzani kuishinda CCM, watuhumiwa 57 wanaodaiwa
kodi ya majengo wamefikishwa kwenye baraza la ardhi na nyumba Wilaya ya
Kinondoni na mgodi wa dhahabu Buzwagi kufungwa kutokana na uzalishaji
kushuka.
Waziri wa Nishati na Madini, George Simbachawene
ambae amezungumzia kuhusu wachimbaji wadogo wanaofanya kazi katika
migodi na machimbo pamoja na soko la biashara ya madini nchini pia
kulikuwa na mazungumzo na Mbunge Augustino Mrema ambae amezungumzia Afya yake pamoja na muenendo wa siasa katika jimbo lake.
Bonyeza play hapa chini kusikiliza story zote…
-via millardayo

Note: Only a member of this blog may post a comment.