Simanzi zimetawala katika familia ya mtoto Festo Filbert mwenye miaka 11 iliyopo Majohe kwa Ngosoma, Dar es salaam baada ya mtoto huyo kujinyonga kwa kutumia mkanda wa suruali.
Tukio la kujinyonga kwa mtoto huyo
aliyekuwa akisoma darasa la nne katika shule ya Msingi Pugu limeacha
huzuni kwa majirani na ndugu zake ambao walikuwa karibu na mtoto huyo.
Mtoto huyo alifikia maamuzi hayo juzi
katika maeneo hayo ambapo alikutwa chumbani kwake akiwa amejinyonga na
mwili wake ukiwa umeng’inia kwenye mkanda alioufunga shingoni.
Baadhi ya wananchi waliokuwa wakiishi
karibu na mtoto huyo walisema wameshtushwa na kifo chake kwani kabla ya
kufikia uamuzi huo alionekana akicheza na wenzake.
Walisema jumapili asubuhi alikwenda
kanisani, na aliporudi alikuwa akichezana wenzake lakini walishangazwa
na taarifa za kwamba amefariki baada ya kuamua kujinyonga.
Hata hivyo haikuwa rahisi kufahamu
sababu za kuamua kujinyonga na sasa maiti yake imehifadhiwa katika
hospitali ya Amana huku upelelezi wa Polisi ukiendelea


Note: Only a member of this blog may post a comment.