Sunday, April 5, 2015

Anonymous

BASTOLA YAZUA KIZAAZAA KANISANI JIJINI DAR

Hofu imewakumba waumini wa Kanisa Katoliki Kisarawe baada ya muumini mmoja kukutwa akiwa na bastola na risasi nane katikati ya ibada.

Polisi pamoja na waumini walitoa taarifa kwamba mwanaume huyo hakuwa muumini wa kanisa hilo na alikuwa akipanga kufanya uhalifu.

Waumini wa kanisa hilo wamesema jamaa huyo aliingia mapema kabla ya ibada kuanza, baadaye akawa anahamahama na mara nyingine alikuwa akitoka nje kufanya mawasiliano.
Ni mara ya kwanza kutokea kwa tukio kama hili na hatujajua alikuwa na lengo gani”—alisema Padri wa Kanisa hilo, Padri Kirimo. 

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Urich Matei amesema mtuhumiwa huyo alikutwa na bastola pamoja na risasi nane, Jeshi la Polisi linamshikilia kwa mahojiano zaidi.
Kamanda Matei amesema mtuhumiwa maelezo ya awali amesema kwamba yeye ni mkazi wa Mburahati na wakati mwingine amesema ni mkazi wa Mkuranga na kazi yake ni mkandarasi.
-MWANANCHI

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.