Hofu imewakumba waumini wa Kanisa
Katoliki Kisarawe baada ya muumini mmoja kukutwa akiwa na bastola na
risasi nane katikati ya ibada.
Polisi pamoja na waumini walitoa taarifa kwamba mwanaume huyo hakuwa muumini wa kanisa hilo na alikuwa akipanga kufanya uhalifu.
Waumini wa kanisa hilo wamesema jamaa huyo aliingia mapema kabla ya ibada kuanza, baadaye akawa anahamahama na mara nyingine alikuwa akitoka nje kufanya mawasiliano.
Waumini wa kanisa hilo wamesema jamaa huyo aliingia mapema kabla ya ibada kuanza, baadaye akawa anahamahama na mara nyingine alikuwa akitoka nje kufanya mawasiliano.
“Ni mara ya kwanza kutokea kwa tukio kama hili na hatujajua alikuwa na lengo gani”—alisema Padri wa Kanisa hilo, Padri Kirimo.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Urich Matei amesema mtuhumiwa huyo alikutwa na bastola pamoja na risasi nane, Jeshi la Polisi linamshikilia kwa mahojiano zaidi.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Urich Matei amesema mtuhumiwa huyo alikutwa na bastola pamoja na risasi nane, Jeshi la Polisi linamshikilia kwa mahojiano zaidi.
Kamanda Matei amesema
mtuhumiwa maelezo ya awali amesema kwamba yeye ni mkazi wa Mburahati na
wakati mwingine amesema ni mkazi wa Mkuranga na kazi yake ni mkandarasi.
-MWANANCHI
Note: Only a member of this blog may post a comment.