Thursday, December 22, 2016

Unknown

Vanessa Mdee atembelea Mapiramidi ya Misri (+Pichaz)

Hujaifaidi Misri kama hujatembelea Mapiramidi ya kihistoria yaliyopo nchini humo. Ndicho alichokifanya Vanessa Mdee baada ya kuzulu katika nchi hiyo.  
Vee Money ameshare picha tatu akiwa katika eneo la Mapiramidi hayo na kuelezea namna alivyojisikia kuyaona kwa mara ya kwanza.
 “I went on a one man tour of the Pyramids of Egypt today. Ticked that right off my bucket list. This picture describes EXACTLY how I feel. REJUVENATED! #CashMadame #Afrika #Egypt #Pyramids #SheKing,” ameandika Vanessa kwenye picha aliyoiweka Instagram.
 “Our ancestors were the original shapers of every thought process that make up our whole design today. Our sophistication and innovation dates back to over 7000 years ago, I was reminded today. Yet we lag behind.We need to reclaim our thrones,” ameandika kwenye picha nyingine.

Kuna takriban Mapiramidi 118 au 138 nchini Misri, kwa mujibu wa Wikipedia na mengi yalijengwa kutumika kama makaburi kwaajili ya Mafarao na wake zao enzi za kale.
Mapiramidi ya kwanza kabisa yanapatikana kwenye mji wa Saqqara, kaskazini magharibi mwa Memphis. Miongoni mwao ni Piramidi la Djoser lililojengwa kati ya mwaka 2630 BC hadi 2611 BC.

Lakini Mapiramidi maarufu zaidi ya Misri yanapatikana huko Giza, katika vitongoji vya Cairo. Piramidi la Khufu ndilo kubwa zaidi kuliko yote. Ni ajabu pekee la enzi za mababu, lililobaki kati maajabu 7 ya dunia.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.