Thursday, September 15, 2016

Unknown

Joh Makini amshirikisha Falz kwenye ‘Acha Nikupende’

Muziki wa Afrika haujawahi kuunganika kama ulivyo sasa. Akitoka kumshirikisha msanii wa hit ya ‘Omo Alhaji’, Ycee wiki mbili zilizopita, Joh Makini amemshirikisha nyota mwingine wa Nigeria, Falz.

Wawili hao waliopo pamoja kwenye msimu wa nne wa Coke Studio Afrika, walikutana mara ya kwanza Nairobi wiki iliyopita kwenye kurekodi kipindi hicho.

Hata hivyo, wameamua kutoishia hapo. Jumatano, Joh na Falz aliyeshinda tuzo ya BET mwaka huu, waliingia kwenye studio za Wanene Ent. kutayarisha ngoma iitwayo ‘Acha Nikupende.’
“KITU!! #TzNigeriaCollabo It’s a wrap #AchaNikupende feat.@falzthebahdguy beat by @kingluffa #wanenestudios #switchRecords
#GODENGINEERING,
” ameandika Joh kwenye Instagram.
Falz alikuwa Tanzania kwenye ziara ya vyombo vya habari.

-Via Bongo5

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.