Wednesday, February 17, 2016

Anonymous

Ushahidi Mpya: Penati ya MESSI na SUAREZ ni Feki Sio Goli... Soma Zadi Hapa

Moja kati ya habari kubwa weekend iliyopita ni penati ya Lionel Messi na Luis Suarez. Jana nilikupa story kwamba Neymar amelalamika kwamba ilibidi iwe penati yake na Suarez alikimbilia tu kupiga.

Sasa leo kutokana na picha mpya zilizotoka ni kwamba ile penati ilikua feki na imevunja sheria ya upigaji penati. Kitu cha kawaida kila mtu anajua ni kwamba mtu akiwa anapiga penati inatakiwa wachezaji wote wakae nje ya box la kipa hadi pale atakapogusa mpira.
Sasa kwenye hii picha inaonyesha kwamba Suarez alikua ameshaingia ndani ya Box wakati Messi bado hata hajapiga mpira. Kama ilivyotokea kwa Henry na Robert Pires na Messi na Suarez nao wamefanya kosa la kisheria.
Picha hii imeenda viral kwenye mtandao wa twitter na kuonyesha kwamba halikua goli halali kwa mujibu wa sheria za penati.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.