Wednesday, February 17, 2016

Anonymous

CHELSEA Yapokea Kipigo Dhidi ya PSG, Lakini Wamevunja Rekodi Hii ya PSG (+VIDEO)


Hatua ya 16 bora ya michuano ya Klabu Bingwa Ulaya imechezwa usiku wa February 16 kwa michezo miwili kupigwa katika viwanja vya Parc des Princes na Estádio da Luz, michezo miwili iliyopigwa usiku huo ni mchezo, kati ya Benfica dhidi ya Zenit St. Petersburg na mchezo wa PSG dhidi ya Chelsea.

Mchezo kati ya Chelsea dhidi ya PSG, ndio ulikuwa unatajwa kuwa mchezo wenye mvuto zaidi, kwani klabu ya PSG haikuwa na rekodi nzuri katika mechi zao sita, walizowahi kukutana, Chelsea alikuwa kashinda mara mbili, na kufungwa mara moja sare ikiwa ni michezo mitatu. Lakini PSG walikuwa na rekodi ya kutokufungwa katika mechi zake 34 msimu huu ilizocheza katika mashindano.

PSG wamefanikiwa kubebwa na takwimu yao ya kutofungwa msimu huu, kwani wamefanikiwa kuiadhibu Chelsea kwa jumla ya goli 2-1, magoli ya PSG yalifungwa na Zlatan Ibrahimovic dakika ya 19 na Edinson Cavani dakika ya 78, wakati Chelsea walifunga goli la kufutia machozi dakika ya 45 kupitia kwa mnigeria John Obi Mikel, goli la Chelsea limevunja rekodi ya PSG ya kutofungwa goli hata moja katika michuano ya UEFA msimu huu katika dimba lake la nyumbani.
Matokeo ya mechi nyingine

Benfica 1 – 0 Zenit St. Petersburg
Video ya magoli ya mechi ya PSG Vs Chelsea

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.