Usiseme hatuna hela, sema huna hela!
Katika kuhakikisha tabasamu kwenye uso wa mrembo wake Kylie Jenner
halikauki, rapper Tyga amemsurprise kwa kumnunulia gari aina ya Ferrari
482 Italia yenye thamani ya $320,000 ambazo ni zawadi ya shilingi
milioni 665!
Tyga akimkabidhi Kylie ufunguo wa gari alilozawadiwa na kumwacha mdomo wazi
Kylie Jenner ametimiza umri wa miaka 18 Jumatatu hii.
Kwa mujibu wa mtandao wa People, Tyga alimpa mpenzi wake gari hilo
lenye rangi nyeupe kwenye sherehe iliyofanyika huko West Hollywood
iliyohudhuriwa na mastaa kibao.
Mastaa waliohudhuria sherehe hiyo ni pamoja na Kim Kardashian, Kanye West, Khloe, Kourtney, Kendall, Kris na Caitlyn Jenner.

Note: Only a member of this blog may post a comment.