Sunday, August 2, 2015

Anonymous

HATIMAYE ARSENAL WENGER AKATA MZIZI WA FITINA....TATHMINI YA MCHEZO HII HAPA!

Pazia la ligi kuu ya England limefunguliwa leo rasmi kwa mchezo wa kugombea taji la ngao ya hisani ya FA – mechi ambayo inawakutanisha washindi wa kombe la Barclays Premier League na mshindi wa kombe la FA au League Cup.
 
Mchezo wa Ngao ya hisani mwaka huu umewakutanisha mahasimu wa jiji la London – Chelsea dhidi ya Arsenal, na matokeo ya mchezo huo ni ushindi kwa vijana wa Arsene Wenger.
  Goli la ushindi lilofungwa kipindi cha kwanza na Alexander Chamberlain lilitosha kuwapa Arsenal ushindi muhimu dhidi ya Chelsea.
Pia siku ya leo imekuwa nzuri kwa kocha Wenger ambaye leo ndio mara ya kwanza ameweza kupata ushindi dhidi ya timu anayoiongoza Jose Mourinho.
Ligi kuu ya Uingereza itaanza rasmi wikiendi ijayo.

USIPITWE! JIUNGE NASI FACEBOOK

Subscribe to this Blog via Email :

TOA MAONI YAKO HAPA (MATUSI HAYARUHUSIWI)

Note: Only a member of this blog may post a comment.