ALIYEKUWA Waziri wa Nishati na Madini,
Profesa Sospeter Muhongo (pichani juu) naye ametangaza nia ya kuwania
Urais ndani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) akiwa kwenye Ukumbi wa Chuo
Huria huko Musoma mkoani Mara jioni hii.
Prof. Muhongo amesema hawezi kutoa ahadi ya
mishahara wakati hajakuza uchumi, hawezi kutoa ahadi ya kujenga shule
wakati hajakuza uchumi hivyo atakuza kwanza uchumi kama ilivyo kauli
mbiu yake ya 'Tukuze Uchumi, Tuondoe Umasikini.'
Katika hotuba yake, Prof. Muhongo amejikita sana katika takwimu na jinsi ya kuinua uchumi wa Taifa na kuondoa umasikini.

Note: Only a member of this blog may post a comment.