Imekuwa utamaduni wa klabu mbalimbali barani ulaya kuzindua jezi mpya
kila msimu ambapo jezi hizi huingia sokoni na kuuzwa kwa mashabiki wa
klabu husika huku klabu hiyo ikijiingizia kipato ambacho husaidia kwenye
uendeshaji wa shughuli zake .
Manchester United inatarajiwa kuzindua jezi mpya siku za hivi
karibuni ambapo zitakuwa jezi ambazo zimetengenezwa na mdhamini mpya wa
klabu hii ambaye ni Adidas . Adidas wameingia mkataba na United baada ya
klabu hiyo kumaliza mkataba wake wa muda mrefu na kampuni ya Nike
Jezi mpya za United zitakazotumika msimu ujao zimevuja kwenye mtandao
wa Internet ambapo picha ya mchezaji Ashley Young imeonekana ambapo
mchezaji huyo ni kama amepozi akiwa anapigwa picha maalum kwa ajili ya
matangazo ya jezi hizo .
Hata hivyo United haijatoa taarifa rasmi kuhusu uzinduzi wa jezi mpya
na kilichoonekana ni picha ambayo wengi wameihusisha na jezi ambazo
United itazindua siku za karibuni .

Note: Only a member of this blog may post a comment.