GEORGE Saguda ambaye mchumba wake, marehemu Rachel
Haule ‘Recho’ wiki iliyopita alitimiza mwaka mmoja kaburini, anadai
kutokewa na mzimu wake ukimueleza mambo mbalimbali hasa akiwa katika
wakati mgumu.
Marehemu Rachel Haule ‘Recho’.
Akipiga stori na gazeti hili, Saguda alisema tangu alipofariki
mchumba wake amekuwa akiishi kwa mateso kwani amejaribu kuwa na mwanamke
mwingine ili kupoteza mawazo lakini imeshindikana.“Mzimu wa Recho hivi sasa unanitokea mara kwa mara hasa nikiwa kwenye wakati mgumu, anakuja na kunielekeza jinsi ya kufanya ili kulitatua tatizo husika ambapo kweli huyafuata na kujikuta nikiwa fresh,” alisema Saguda.

Note: Only a member of this blog may post a comment.